Ajinyonga Baada Ya Kunyimwa Tendo La Ndoa Na Mkewe…Soma Zidi Hapa!


Joseph Ojur mwenye miaka 52 mkazi wa ukanda wa  Kabagu katika manispaa ya Njeru amejinyonga mpaka kufa jumapili ya June 3 baada ya kunyimwa ‘unyumba’ na mkewe.

Ojur anasemekana kumwambia mkewe kuwa alifanya vipimo vya ugonjwa wa UKIMWI na akakutwa nao. Na tangu amwambie mkewe hivyo amekuwa akinyimwa ‘unyumba’.

Kamamnda wa Polisi eneo la Njeru, Christopher Tuhunde amesema kuwa, marehemu alijinyonga ndani ya nyumba yake na jeshi hilo linaendelea kuchunguza kwa undani juu ya tukio hilo ili kuja na ripoti kamili kuhusiana na kujinyonga kwa Ojur.

Hata hivyo Tuhunde amewashauri wakazi wa eneo hilo kupenda kuomba ushauri kwa wenzao juu ya matatizo yanayowakabili kuliko kukimbilia kujiua.
Ajinyonga Baada Ya Kunyimwa Tendo La Ndoa Na Mkewe…Soma Zidi Hapa! Ajinyonga Baada Ya Kunyimwa Tendo La Ndoa Na Mkewe…Soma Zidi Hapa! Reviewed by Admin on Tuesday, June 05, 2018 Rating: 5

No comments:

DONDOSHA COMENT YAKO HAPA

Powered by Blogger.